Ijumaa, 23 Desemba 2016

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe Hashim Mgandilwa ametembelea miradi ya maendelea katika kata mbalimbali na kutoa ushauri na kushiriki katika Ujenzi.

Mkuu wa Wilaya Mhe. Hashim Mgandilwa akijaza kifusi katika ujenzi wa darasa shule ya Msingi Kisiwani

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Hashim Mgandilwa (watatu kushoto) akikagua miradi

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Hashim Mgandilwa akikagua ujenzi wa choo katika shule ya Sekondari Mianzini

MKUU WA WILAYA YA KIGAMBONI AONGEA NA WATUMISHI 


Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Hashim Mgandilwa ameitisha kikao cha watumishi kwa lengo la kujitambulisha pia kuwaasa watumishi wafanye kazi kwa bidii.

Akiongea na watumishi Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni aliwapongeza watumishi kwa kuanzisha Halmashauri mpya pia kasi walioanza nayo waendelee nayo.

''Nawapongeza sana kwa kuchaguliwa kuja Kigamboni. Fanyeni kazi, taarifa zitolewe kwa wakati na kazi zifanyike. Kama huna jibu la swali la mteja mwambie ukweli na si kumsumbua au kumdanganya.Fanyeni kazi, acheni mambo ya kukaa ofisini, tokeni nje ili kujua shida za wananchi'' Alisema Mgandilwa.

Pia alisema kuwa Kigamboni ni eneo pekee katika Jiji la Dar es Salaam linaloendelezwa, hivyo kuna haja ya kupanga vizuri. Aliwaagiza watumishi wa ardhi  kusimami, kuzuia migogoro ya ardhi na kuuza kiwanja kwa watu wawili tofauti.

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Hashim Mgandilwa


Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni Bw. Stephen  E. Katemba

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Bw. Hashim Mgandilwa akiongea na watumishi (hawapo pichana)

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni  Bw. Hashim Mgandilwa (wakwanza kulia) akifuatiwa na Katibu Tawala wa Wilaya Bibi Rachel Mhando  na Kaimu Mkuu wa Idara ya  Utumishi na Utawala Bibi Paulina Siara   

Watumishi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni wakiwa kwenye mkutano wa Mkurugenzi na Mkuu wa Wilaya (hawapo pichani)

Watumishi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni wakimsikiliza Mkurugenzi wa Halmashauri (hayupo pichani)

Jumatatu, 10 Oktoba 2016

Mkuu wa Wilaya azindua kampeni ya Mti wangu.

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Hashim Mgandilwa amezindua siku ya upandaji mti Kiwilaya ambapo Kimkoa ilizinduliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ikiwa na kauli mbiu "MTI WANGU"

Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni imepanda jumla ya miti 1650 na zoezi hili ni endelevu lengo likiwa ni kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Bw. Hashim Mgandilwa (kushoto) akibadilishana mawazo na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bw. Stephen Katemba siku ya upandaji mti" MTI WANGU"

Jumapili, 9 Oktoba 2016

Mstahiki Meya wa Jiji la Dar Es Salaam Isaya Mwita  (wa kwanza kulia) akipanda mti katika eneo la daraja la Mwalimu Nyerere siku ya upandaji mti

Mbunge wa Kigamboni Mhe. Faustine Ndungulile akimwagilia mti alioupanda siku ya Upandaji mti huku akishuhudiwa na watumishi wa Halmashauri ya Kigamboni na wananchi

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni  Bw. Hashim Mgandilwa akipanda mti wake

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni Bw. Stephen Katemba akimwagilia mti wake 

Pamoja tunaweza 

Watumishi wa NSSF wakiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya Bw. Hashim Mgandilwa na Mkurugenzi wa Halmashauri Bw. Stephen Katemba siku ya kupanda miti. 

Mbunge wa Kigamboni Mhe. Faustine Ndungulile akiwasalimia wananchi waliojitokeza kupanda miti

Alhamisi, 6 Oktoba 2016

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni Bw. Stephen Katemba akiongea na halaiki cku ya upandaji mti(Mti wangu) eneo la Daraja la Mwalimu Nyerere. Kushoto kwake ni Katibu Tawala wa Halmashauri Bibi Rachel Mhando

Jumatatu, 12 Septemba 2016

Mkuu wa Wilaya akiongea na jumuia ya Mtaa wa Feri (Tandavamba)

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Hashim Mgandilwa amefanya mkutano na wamiliki wa Boti,wavuvi, mafundi friji,mafundi mashine za boti,mama lishe, wafanya biashara wa vioski, wauza maji na kahawa wa mtaa wa Feri (Tandavamba), lengo kuu likiwa ni kujitambulisha. Kutokana na mazingira mabaya ya sehemu wanayojipatia riziki umoja huo, Mgandilwa aliahidi kuwa litajengwa Soko la Kimataifa la Samaki ambalo pia litakuwa chanzo kikuu cha mapato katika Wilaya ya Kigamboni.
Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Hashim Mgandilwa akiongea na wakazi wa mtaa wa Feri - Tandavamba 

Mkurugenzi akiwa Tandavamba

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni Bw. Stephen Katemba akijitambulisha kwa wakazi wa Mtaa wa Feri (Tandavamba) pia aliwaahidi kutekeleza yale yote yatakayoelekezwa na Mkuu wa Wilaya kwani yeye ndio Mtendaji katika Halmashauri.

Diwani wa Kata ya Kigamboni

Diwani wa Kata ya Kigamboni Mhe. Dotto Msawa akiwasalimia  wafanyabiashara wa Mtaa wa Feri (Tandavamba)  katika kikao cha Mkuu wa Wilaya hiyo alipoenda  kuwasalimia wananchi wa eneo hilo

Changamoto Sokoni


Utambuzi wa Mipaka ya Soko la Urassa



Mtendaji wa Kata ya Kigamboni Bw. Msafiri Munna (katikati) akionyesha mipaka ya soko la Urassa kwa timu ndogo iliyokuwa imeambatana na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kigamboni Bw. Stephen Katemba (wapili kulia). Soko hili limezungukwa na majengo mbalimbali yakiwemo maduka na nyumba za kuishi


Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni ametembelea soko la Urassa

Jumapili, 11 Septemba 2016

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni Bw. Stephen Katemba ameongea na watumishi wa Halmashauri hiyo mara baada ya kufika kuripoti katika Ofisi za Halmashauri zilizopo katika kata ya Mjimwema.  Bw. Katemba aliwapongeza sana watumishi kwa kukubali kufika Ofisini kuripoti na aliwaambia kuwa hiyo ni bahati na nafasi ya pekee kwao kwa kuteuliwa kuwa waanzilishi wa ofisi."Hongereni sana, hiyo ni opportunity kubwa ya kuanzisha ofisi mpya ya Kigamboni hivyo onyesheni ufanisi wenu.Mimi nawategemea sana, fanyeni kazi kwa bidii. Tunataka mabadiliko, hatutaki wafanyakazi wanaofanya kazi kwa kubabaisha, toa huduma kwa wakati na useme ukweli wakati wote. " Alisema Katemba.


Watumishi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni wakimsikiliza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bw. Stephen Katemba(hayupo pichani) wakati akijitambulisha.








Ijumaa, 2 Septemba 2016

Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar Es Salaam Bibi Theresia Mmbando (wa kwanza kulia) akiongea na watumishi wapya wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni mara baada ya kuripoti Ofisini. Katibu Tawala aliwapongeza watumishi hao kwa kupata kituo kipya cha kazi na kuwaasa wafanye kazi kwa weledi na ufanisi wa hali ya juu.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni Bw. David Mgonja akizungumza na Watumishi wapya wa Halmashauri ya Kigamboni kabla ya kumkaribisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar Es Salaam Bibi Theresia Mmbando. Watumishi hawa ni matokeo ya Mgawanyo wa watumishi wa Temeke Manispaa ambao baadhi yao wamehamishiwa Halmashauri ya Kigamboni

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni Bw. David Mgonja (katikati) akimuonyesha Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar Es Salaam  Bibi Theresia Mmbando sehemu ya Ofisi ya Mkurugenzi

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Bw. Hashim Mgandilwa(Kushoto) akisalimiana na Bibi Theresia Mmbando Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar Es Salaam alipokwenda kuangalia ofisi mpya ya Wilaya ya Kigamboni
  
  

  
  

Jumatatu, 29 Agosti 2016

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni Bw. Stephen Katemba(aliyevaa taji) akiwa katika picha ya pamoja na vijana wa Mjimwema Jogging mara baada ya kufanya usafi katika Zahanati ya Mji Mwema.


Jumatatu, 15 Agosti 2016

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni na Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni wametembelea kituo cha kulea wazee wasiojiweza kilichopo Nunge katika Wilaya ya Kigamboni.Wakiwa kituoni hapo walizungumza na wazee waliopo katika kituo hicho na kutoa onyo kali kwa wale ambao huuza vitu wanavyopewa kama msaada kituoni hapo.
Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Hashim Mgandilwa  (mwenye Baragashia) pamoja na Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni wa kwanza kushoto Bw Stephen Katemba wakiukabidhi uongozi wa kituo cha kulea wazee wasiojiweza msaada wa vitu mbalimbali.