Alhamisi, 27 Julai 2017

WAZEE 2376 WAPATIWA VITAMBULISHO VYA MATIBABU BURE




Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy  Ally Mwalimu

Waziri wa Afya ,Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,wazee na watoto Mh. Ummy Mwalimu amekabidhi zaidi ya vitambulisho 2300 kwa wazee wa Manispaa ya Kigamboni kwa ajili ya kuwawezesha kupata matibabu bila malipo katika hospitali zote za Manispaa ya Kigamboni.

Zoezi la utoaji vitambulisho hivyo limefanyika katika Hospitali ya Wilaya ya Kigamboni ( Vijibweni) na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali wa manispaa ya kigamboni wakiongozwa na mkuu wa Wilaya Mh. Hashim Mgandilwa.

Viongozi wengine waliohudhurio hafla hiyo ni pamoja na Meya wa manispaa ya Kigamboni Mh.Maabad Suleiman Hoja ,Waheshimiwa madiwani pamoja na Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni ndg Stephen Katemba.

Akisoma risala mbele ya mgeni Rasmi Ndg Katemba alisema wazee hao 2376 ni sehemu ya wazee 7000 wanaotarajiwa kunufaika na mpango huo kwani mpaka sasa zoezi la kuwatambua linaendelea chini ya usimamizi wa idara ya Ustawi na maendeleo ya Jamii wa Manispaa ya Kigamboni.

Mkurugenzi aliongeza kuwa ,kuanzia sasa hatarajii kuona wazee wakipata tabu ya matibabu kwani mpango huo unawawezesha kupata matibabu yote bure kuanzia vipimo mpaka kumuona Daktari.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy  Ally Mwalimu akimkabidhi kitambulisho cha matibabu Mzee Jafary Said Said.


Picha ya pamoja
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy  Ally Mwalimu akiongea na wananchi

















Hakuna maoni:

Chapisha Maoni