Jumatano, 6 Desemba 2017

TBA KUJENGA OFISI ZA MANISPAA








Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni Ndg. Stephen Katemba pamoja na Mtendaji mkuu wa wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Ndg Eliud Mwakalinga wametia saini ya mkataba wa ujenzi wa ofisi ya Halmashauri ya Manispaa kuanzia Januari 2018.Ujenzi huo wa ofisi unatajiwa kuchukua miezi Minane na unatarajiwa kukamilika mwezi wa tisa mwaka 2018.

Kukamilika kwa ujenzi huo kutaondoa usumbufu kwa watumishi na wananchi wanaofika kupata huduma kutokana na ofisi za Idara mbali mbali kuwa sehemu tofauti tofauti  hivyo kuwalazimu wananchi na watumishi kusafiri toka ofisi moja kwenda nyingine.
Kwa upande wa rasilimali ,Halmashauri itaokoa zaidi ya shilingi milioni 30 zinazotumika kulipia ofisi za Manispaa katika majengo ya watu binafsi kwa Mwaka.Mtendaji mkuu wa TBA Ndg. Mwakalinga alimuhakikishia Mkurugenzi kuwa wanakabidhi jengo kwa muda waliokubaliana kwenye mkataba.

 

Maoni 3 :