Jumapili, 11 Septemba 2016

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni Bw. Stephen Katemba ameongea na watumishi wa Halmashauri hiyo mara baada ya kufika kuripoti katika Ofisi za Halmashauri zilizopo katika kata ya Mjimwema.  Bw. Katemba aliwapongeza sana watumishi kwa kukubali kufika Ofisini kuripoti na aliwaambia kuwa hiyo ni bahati na nafasi ya pekee kwao kwa kuteuliwa kuwa waanzilishi wa ofisi."Hongereni sana, hiyo ni opportunity kubwa ya kuanzisha ofisi mpya ya Kigamboni hivyo onyesheni ufanisi wenu.Mimi nawategemea sana, fanyeni kazi kwa bidii. Tunataka mabadiliko, hatutaki wafanyakazi wanaofanya kazi kwa kubabaisha, toa huduma kwa wakati na useme ukweli wakati wote. " Alisema Katemba.


Watumishi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni wakimsikiliza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bw. Stephen Katemba(hayupo pichani) wakati akijitambulisha.








Hakuna maoni:

Chapisha Maoni