Jumatatu, 12 Septemba 2016

Mkuu wa Wilaya akiongea na jumuia ya Mtaa wa Feri (Tandavamba)

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Hashim Mgandilwa amefanya mkutano na wamiliki wa Boti,wavuvi, mafundi friji,mafundi mashine za boti,mama lishe, wafanya biashara wa vioski, wauza maji na kahawa wa mtaa wa Feri (Tandavamba), lengo kuu likiwa ni kujitambulisha. Kutokana na mazingira mabaya ya sehemu wanayojipatia riziki umoja huo, Mgandilwa aliahidi kuwa litajengwa Soko la Kimataifa la Samaki ambalo pia litakuwa chanzo kikuu cha mapato katika Wilaya ya Kigamboni.
Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Hashim Mgandilwa akiongea na wakazi wa mtaa wa Feri - Tandavamba 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni