Jumatatu, 31 Julai 2017

VITUO VYA AFYA VYAPATA ALAMA ZA JUU

Mkurugenzi Bw. Stephen Katemba (kulia) akipokea taarifa kutoka kwa Bi. Ruth Ngowi          





Katika ukaguzi wa Kimaabara uliofanywa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa mwaka 2017 ,Vituo vya Afya katika Manispaa ya Kigamboni vimeonekana kuwa na alama za juu katika kutoa huduma kwa Jamii.
Katika kaguzi huo ulioongozwa na Bi.Ruth Ngowi,Jumla ya vituo vya Afya 13 vimepata alama za nyota Tatu  na zaidi ikiwa ni kiashiria kuwa huduma zinazotolewa ni bora na za kuridhisha.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni alikabidhiwa ripoti hiyo na timu ya ukaguzi na kuahidi kuendelea kusimamia ubora zaidi kwani kwa upande wa vituo vya Afya vilivyo chini yake vilikuwa na alama 76 tofauti na alama za jumla za 48 inayounganisha vituo vya serikali na vya Binafsi.
Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni ina Jumla ya Vituo vya Afya 27,kati ya hivyo 17 ni vya serikali na 10 ni vya watu binafsi na mashirika mbali mbali.

Picha ya pamoja ya watumishi wa Halmashauri na Wizara

Alhamisi, 27 Julai 2017

WAZEE 2376 WAPATIWA VITAMBULISHO VYA MATIBABU BURE




Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy  Ally Mwalimu

Waziri wa Afya ,Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,wazee na watoto Mh. Ummy Mwalimu amekabidhi zaidi ya vitambulisho 2300 kwa wazee wa Manispaa ya Kigamboni kwa ajili ya kuwawezesha kupata matibabu bila malipo katika hospitali zote za Manispaa ya Kigamboni.

Zoezi la utoaji vitambulisho hivyo limefanyika katika Hospitali ya Wilaya ya Kigamboni ( Vijibweni) na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali wa manispaa ya kigamboni wakiongozwa na mkuu wa Wilaya Mh. Hashim Mgandilwa.

Viongozi wengine waliohudhurio hafla hiyo ni pamoja na Meya wa manispaa ya Kigamboni Mh.Maabad Suleiman Hoja ,Waheshimiwa madiwani pamoja na Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni ndg Stephen Katemba.

Akisoma risala mbele ya mgeni Rasmi Ndg Katemba alisema wazee hao 2376 ni sehemu ya wazee 7000 wanaotarajiwa kunufaika na mpango huo kwani mpaka sasa zoezi la kuwatambua linaendelea chini ya usimamizi wa idara ya Ustawi na maendeleo ya Jamii wa Manispaa ya Kigamboni.

Mkurugenzi aliongeza kuwa ,kuanzia sasa hatarajii kuona wazee wakipata tabu ya matibabu kwani mpango huo unawawezesha kupata matibabu yote bure kuanzia vipimo mpaka kumuona Daktari.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy  Ally Mwalimu akimkabidhi kitambulisho cha matibabu Mzee Jafary Said Said.


Picha ya pamoja
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy  Ally Mwalimu akiongea na wananchi

















Jumatano, 26 Julai 2017

NAFASI ZA KAZI



Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni imepokea kibali Kumb. Na. FA 170/374/01/27 cha tarehe 14 Julai, 2017 kutoka kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Kibali Kumb. Na. FA.102/282/02B/13 cha tarehe 30 Juni, 2017 kutoka kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI). Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni anawatangazia wananchi wote raia wa Tanzania wenye sifa kuomba nafasi zilizoorodheshwa hapo chini.

1.     MTENDAJI WA MTAA DARAJA LA III-  (NAFASI 31)
(a)   Sifa za Mwombaji
Kuajiriwa mwenye Elimu ya Kidato cha Nne (IV) au Sita (VI) aliyehitimu mafunzo ya Astashahada/Cheti katika moja ya fani zifuatazo: Utawala, Sheria, Elimu ya Jamii, Usimamizi wa Fedha, Maendeleo ya Jamii na Sayansi ya Sanaa kutoka Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo, Dodoma au Chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali.
Kazi na majukumu ya Mtendaji wa Mtaa
(a)   Katibu wa kamati ya Mtaa
(b)   Mtendaji Mkuu wa Mtaa
(c)   Mratibu wa utekelezaji wa Sera na Sheria zinazotekelezwa na Halmashauri katika Mtaa
(d)   Mshauri wa Kamati ya Mtaa kuhusu Mipango ya Maendeleo katika Mtaa
(e)   Msimamizi wa Utekelezaji wa Sheria ndogo pamoja na Sheria nyingine zinazotumika katika Mtaa
(f)    Mshauri wa Kamati ya Mtaa kuhusu masuala ya Ulinzi na Usalama
(g)   Msimamizi wa utekelezaji wa mikakati mbalimbali inayohusu uondoaji wa njaa na Umaskini katika Mtaa
(h)   Kusimamia ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri na kutunza kumbukumbu za walipa kodi wote
(i)     Kuandaa na kutunza rejesta ya wakazi wote wa Mtaa
(j)     Atawajibika kwa Mtendaji wa Kata

       Ngazi ya mshahara ni TGS B sawa na Shilingi 390,000/= kwa mwezi

2.     MTUNZA KUMBUKUMBU MSAIDIZI DARAJA LA II  (NAFASI 5)
(a)   Kuajiriwa mwenye Elimu ya Kidato cha Nne (IV) au cha Sita (VI) waliohudhuria mafunzo ya Utunzaji wa Kumbukumbu nakupata cheti cha NTA LEVEL 5 katika mojawapo ya fani za Afya,Masjala, Mahakama na Ardhi

Kazi na Majukumu
(a)   Kutafuta kumbukumbu/nyaraka/mafaili yanayohitajiwa na wasomaji
(b)   Kudhibiti upokeaji, uandikishaji wa kumbukumbu/ nyaraka
(c)   Kuweka/kupanga kumbukumbu/nyaraka katika reki (file racks/cabinets) katika masjala/vyumba vya kuhifadhia kumbukumbu
(d)   Kuweka kumbukumbu (barua,nyaraka n.k) katika mafaili
(e)   Kushughulikia maombi ya kumbukumbu/nyaraka kutoka Taasisi za Serikali

          Ngazi ya mshahara ni TGS B sawa na Shilingi 390,000/= kwa mwezi

3.     KATIBU MAHSUSI DARAJA LA III   (NAFASI 1)
(a)   Kuajiriwa mwenye Elimu ya Kidato cha Nne (IV) waliohudhuria mafunzo ya Uhazili nakupata cheti cha NTA LEVEL 5. Wawe wamefaulu somo la hati mkato ya Kiswahili na Kiingereza maneno 80 kwa dakika moja na wawe wamepata mafunzo ya kutumia kompyuta kutoka Chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali nakupata Cheti katika programu za Windows,Microsoft Office,Internet,E-mail na Publisher.

     KAZI NA MAJUKUMU YA KATIBU MAHSUSI DARAJA LA III  
(a)   Kuchapa barua, taarifa na nyaraka za kawaida
(b)   Kusaidia kupokea wageni na kuwasaili shida zao, na kuwaelekeza sehemu wanapoweza kushughulikiwa
(c)   Kusaidia kutunza taarifa/kumbukumbu za matukio, miadi, wageni, tarehe za vikao, safari za mkuu wake na ratiba za kazi nyingine zilizopangwa kutekelezwa katika Ofisi anayofanyia kazi na kumuarifu mkuu wake kwa wakati unaohitajika
(d)   Kusaidia kutafuta na kumpatia Mkuu wake majalada, nyaraka au kitu chochote kinachohitajika katika shughuli za hapo Ofisini
(e)   Kusaidia kufikisha maelekezo ya Mkuu wake wa kazi kwa wasaidizi wake na pia kumuarifu kuhusu taarifa zozote anazokuwa amepewa na wasaidizi hao
(f)    Kusaidia kupokea majalada, kuyagawa kwa Maofisa walio katika Sehemu alipo, na kuyakusanya, kuyatunza na kuyarudisha sehemu zinazohusika
(g)   Kutekeleza kazi zozote atakazokuwa amepangiwa na Msimamizi wake wa kazi

    Ngazi ya mshahara ni TGS B sawa na Shilingi 390,000/= kwa mwezi

4.     MSAIDIZI WA HESABU     (NAFASI 2)
(a)   Kuajiriwa wenye Cheti cha ATEC level II au “Foundation Level” kinachotambuliwa na NBAA, waombaji wawe na uzoefu wa kazi zaidi ya mwaka (1) katika fani hiyo

  KAZI NA MAJUKUMU YA MSAIDIZI WA HESABU.
(a)   Kuandika na kutunza “register”zinazohusu shughuli za uhasibu
(b)   Kuandika hati za malipo na hati za mapokezi ya fedha
(c)   Kutunza majalada yenye kumbukumbu za hesabu
(d)   Kupeleka barua/ nyaraka za Uhasibu benki Kufanya usuluhisho wa masurufu, karadha, Hesabu za Benki na Amana.

Ngazi ya mshahara ni TGS B sawa na Shilingi 390,000/= kwa mwezi

NB. Kwa nafasi ya Msaidizi wa Hesabu itakuwa ni kwa Mkataba wa Mwaka mmoja na waombaji wawe tayari kufanya kazi katika Vituo vya Afya.

MASHARTI KWA UJUMLA
1.     Mwombaji awe raia wa Tanzania na awe tayari kufanya kazi sehemu yoyote ya Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni
2.     Mwombaji awe na Umri usiozidi miaka 45 na awe hajawahi kupatikana na kosa lolote la jinai, kufungwa jela au kufukuzwa kazi katika Utumishi wa Umma
3.     Waombaji  waambatishe maelezo yao binafsi (C.V)
4.     Maombi yote yaambatane na nakala ya vyeti vya taaluma, vyeti vya kidato cha (IV au VI), cheti cha kuzaliwa na picha mbili za rangi za hivi karibuni na ziandikwe majina nyuma
5.     “Testemonials, provisional results, Statment of Results hati ya matokeo ya kidato cha nne na sita (FORM IV and FORM VI RESULT SLIPS) HAVITAKUBALIWA
6.     Waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe vyeti vyao vimehakikiwa na kuidhinishwa na Mamlaka husika TCU na NACTE na taarifa ya uhakiki iambatishwe kwenye maombi
7.     Uwasilishwaji wa taarifa na sifa za kugushi wahusika watachukuliwa hatua za kisheria
8.     Barua zote za maombi ziandikwe kwa mkono
9.     Mwisho wa kupokea barua za Maombi ni tarehe 15.08.2017 saa 9:30 alasiri.

Maombi yatumwe kwa Anuani ifuatayo:

Mkurugenzi,
Halmashauri ya Manispaa Kigamboni,
S.L.P 36009,
Kigamboni, Dar es Salaam.