Jumatano, 11 Oktoba 2017

PIMA AFYA BURE

Mkurugenzi wa Halmashauri anawakaribisha wananchi wote kufika katika viwanja vilivyopo karibu na ofisi za Halmashauri kuanzia tarehe 10/10/2017 hadi 15/10/2017 kwa ajili ya kupima afya. Huduma zitolewazo ni pamoja na kupima maambukizi ya virusi vya ukimwi, shinikizo la damu,Kisukari, Saratani kwa akina mama/baba (Huduma inatolewa katika Hospitali ya Vijibweni) na Tezi dume.(Huduma inatolewa katika Hospitali ya Vijibweni)


 KARIBUNI SANA.

WAKAZI WA KIGAMBONI WAKIPATIWA HUDUMA





KARIBUNI SANA KUWEKEZA KIGAMBONI

Wageni mbalimbali wameendelea kumiminika kwa ajili ya kuwekeza katika Halmashauri yetu. Karibuni sana wote kwani Tanzania ya viwanda kigamboni inawezekana.

Mkurugenzi wa Halmashauri Bw. Stephen E. Katemba (katikati) akiwa na wawekezaji

MAFUNZO YA PLANREP

Wakuu wa Idara/ Vitengo na Maafisa Bajeti wamepewa mafunzo juu ya utumiaji wa mfumo mpya wa uandaaji wa bajeti (PLANREP) ya Halmashauri na Mkufunzi wa ndani Bw. Masore Masogo - Mtakwimu Mkuu.