Jumanne, 22 Agosti 2017

MKURUGENZI AFUNGA SHULE 18 ZISIZOSAJILIWA


Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni ndg. Stephen Katemba ametoa agizo la kufungwa kwa shule zote za Awali,Msingi na Sekondari za binafsi zisizo na usajili na zile zenye mazingira hatarishi kwa wanafunzi.


Zoezi hilo lililoanza leo tarehe 22 Agosti 2017 limepanga kufunga shule 58 za awali na msingi ambazo mpaka sasa zimebainika kutokuwa na usajili wa aina yoyote huku zikiendelea kutoa elimu pamoja na kuwa walishapewa barua toka Januari 2017 ikiwataka kutopokea wanafunzi mpaka hapo watakapokamilisha usajili.

Ofisi ya Afisa elimu Manispaa ya Kigamboni ikishirikiana na wakaguzi wa ubora wa elimu ilipewa jukumu la kupita shule hadi shule na kuzifunga kwa niaba ya Mkurugenzi endapo zitakuwa hazijakidhi  vigezo vya kutoa elimu. 

Msimamizi wa zoezi hilo Kaimu Afia elimu Msingi Mwl. Mathew Komba alisema zoezi hili litaendelea kwa siku tano mfululizo ambapo kwa siku ya kwanza zoezi lilifanyika katika kata tatu za Vijibweni,Kigamboni na Tungi ambapo shule 18 zilifungwa na wamiliki wa shule hizo kutakiwa kusimamisha zoezi la ufundishaji kuanzia leo tarehe 22 Agosti na endapo watakaidi hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Baadhi ya shule zilizofungwa ni pamoja na shule ya awali ya Malaika, Kigamboni English Medium school, Patmos ,Montecalos pamoja na Riziki. Zingine ni Taqwa ,Fildaus ,Mek na Charity.
Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni Ndg Stephen Katemba anatoa wito kwa wamiliki wote waliofungiwa shule kutojaribu kufungua shule hizo mpaka hapo ofisi yake itakaporidhika kulingana na maagizo yaliyotolewa.



kaimu Afisa Elimu Msingi Mwalimu Mathew Komba (Katikati) akimpa maelekezo mmiliki wa shule ya Malaika iliyopo kata ya Tungi

Wanafunzi wakiwa wamelala katika mazingira yasiyokubalika na muongozo wa usajili wa shule

Baadhi ya wanafunzi wa Kigamboni Islamik Nursery and Primary school  wakifundishwa katika jengo la Msikiti badala ya darasani

Jumatatu, 21 Agosti 2017

MALIPO YOTE KWA MASHINE YA EFD

Vijana wa Kigamboni wakionesha utaalamu wao wa kutumia mashine ya EFD kwa viongozi wa Wilaya hiyo. Kutoka kulia ni Mkuu wa Wilaya  Mhe. Hashim Mgandilwa na Mkurugenzi Bw. Stephen Katemba



Mkuu wa Wilaya Mhe. Hashim Mgandilwa akiangalia risiti iliyochapishwa kwa mashine ya EFD kama inakidhi mahitaji ya Halmashauri na kuitambulisha kwa ufasaha.

Mkuu wa Wilaya Mhe. Hashim Mgandilwa akionesha mfano wa risiti ya mashine ya EFD ambayo itatumika kwa malipo yote katika Halmashauri

Vijana wanaweza. Viondozi wa Halmashauri(waliovaa t-shirt za rangi ya kijani kibichi wakiangalia kama vijana wanaweza kutumia mashine za EFD kwa ufasaha

Jumapili, 20 Agosti 2017

USAFI KWANZA

Wananchi wa Kigamboni mnatakiwa kufanya usafi kuzunguka maeneo yenu ya makazi na biashara. Ukaguzi utaendelea kufanyika na endapo eneo lako litakuwa chafu, hatua za kisheria zitachukuliwa ikiwemo faini za papo kwa papo.

Vijana wa Kigamboni wakiwa tayari kuingia msituni kupambana na adui takataka. Kigamboni safi ya mfano inakuja

Alhamisi, 3 Agosti 2017

KARIBU KATIKA BANDA LETU MOROGORO

Karibuni sana katika banda letu la maonesho lililopo katika viwanja vya Nane Nane Mkoani Morogoro. Katika banda hili mtajifunza ukulima wa kisasa, ufugaji wa kisasa kwa mifugo ya aina zote na njia mpya za Kilimo biashara na kutambua maeneo ya uwekezaji.

Karibuni sana, sana.


Mstahiki Meya Maabad Suleiman Hoja (Katikati) akiwa na Naibu Meya Mhe. Amin Mzuri Sambo(kulia) na Mkurugenzi Bw. Stephen Katemba