Jumatano, 6 Desemba 2017

TBA KUJENGA OFISI ZA MANISPAA








Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni Ndg. Stephen Katemba pamoja na Mtendaji mkuu wa wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Ndg Eliud Mwakalinga wametia saini ya mkataba wa ujenzi wa ofisi ya Halmashauri ya Manispaa kuanzia Januari 2018.Ujenzi huo wa ofisi unatajiwa kuchukua miezi Minane na unatarajiwa kukamilika mwezi wa tisa mwaka 2018.

Kukamilika kwa ujenzi huo kutaondoa usumbufu kwa watumishi na wananchi wanaofika kupata huduma kutokana na ofisi za Idara mbali mbali kuwa sehemu tofauti tofauti  hivyo kuwalazimu wananchi na watumishi kusafiri toka ofisi moja kwenda nyingine.
Kwa upande wa rasilimali ,Halmashauri itaokoa zaidi ya shilingi milioni 30 zinazotumika kulipia ofisi za Manispaa katika majengo ya watu binafsi kwa Mwaka.Mtendaji mkuu wa TBA Ndg. Mwakalinga alimuhakikishia Mkurugenzi kuwa wanakabidhi jengo kwa muda waliokubaliana kwenye mkataba.

 

Jumatano, 11 Oktoba 2017

PIMA AFYA BURE

Mkurugenzi wa Halmashauri anawakaribisha wananchi wote kufika katika viwanja vilivyopo karibu na ofisi za Halmashauri kuanzia tarehe 10/10/2017 hadi 15/10/2017 kwa ajili ya kupima afya. Huduma zitolewazo ni pamoja na kupima maambukizi ya virusi vya ukimwi, shinikizo la damu,Kisukari, Saratani kwa akina mama/baba (Huduma inatolewa katika Hospitali ya Vijibweni) na Tezi dume.(Huduma inatolewa katika Hospitali ya Vijibweni)


 KARIBUNI SANA.

WAKAZI WA KIGAMBONI WAKIPATIWA HUDUMA





KARIBUNI SANA KUWEKEZA KIGAMBONI

Wageni mbalimbali wameendelea kumiminika kwa ajili ya kuwekeza katika Halmashauri yetu. Karibuni sana wote kwani Tanzania ya viwanda kigamboni inawezekana.

Mkurugenzi wa Halmashauri Bw. Stephen E. Katemba (katikati) akiwa na wawekezaji

MAFUNZO YA PLANREP

Wakuu wa Idara/ Vitengo na Maafisa Bajeti wamepewa mafunzo juu ya utumiaji wa mfumo mpya wa uandaaji wa bajeti (PLANREP) ya Halmashauri na Mkufunzi wa ndani Bw. Masore Masogo - Mtakwimu Mkuu.





Ijumaa, 29 Septemba 2017

MSAADA KWA WAZEE

Mkurugenzi Mkazi wa shirika la World Share la nchini Korea Nara Kim (wanne kutoka kulia) kwenye picha ya pamoja na uongozi wa kituo cha kulelea wazee Nunge walipofika kutoa msaada wa vitu mbalimbali.

BARAZA MAALUMU LA KUPITIA TAARIFA YA UFUNGAJI WA HESABU UNAOISHIA 30 JUNI

Mkutano Maalumu wa Baraza la Madiwani ukiongozwa na Mstahiki Meya Maabad Suleiman Hoja kwa ajili ya  kupitisha  taarifa ya ufungaji wa Mahesabu kwa mwaka unaoishia 30 Juni 2017










Mkurugenzi Bw. Stephen E. Katemba (aliyesimama) akiwasilisha agenda

Viongozi wa Halmashauri wakifuatilia agenda mbalimbali kwa umakini


Waheshimiwa Madiwani wakisikiliza uwasilishaji wa Agenda tayari kwa kuchangia

Mhe. Sanya Bunaye Diwani wa Kata ya Kimbiji (wakwanza kulia) akichangia mada katika mkutano wa baraza


Jumanne, 22 Agosti 2017

MKURUGENZI AFUNGA SHULE 18 ZISIZOSAJILIWA


Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni ndg. Stephen Katemba ametoa agizo la kufungwa kwa shule zote za Awali,Msingi na Sekondari za binafsi zisizo na usajili na zile zenye mazingira hatarishi kwa wanafunzi.


Zoezi hilo lililoanza leo tarehe 22 Agosti 2017 limepanga kufunga shule 58 za awali na msingi ambazo mpaka sasa zimebainika kutokuwa na usajili wa aina yoyote huku zikiendelea kutoa elimu pamoja na kuwa walishapewa barua toka Januari 2017 ikiwataka kutopokea wanafunzi mpaka hapo watakapokamilisha usajili.

Ofisi ya Afisa elimu Manispaa ya Kigamboni ikishirikiana na wakaguzi wa ubora wa elimu ilipewa jukumu la kupita shule hadi shule na kuzifunga kwa niaba ya Mkurugenzi endapo zitakuwa hazijakidhi  vigezo vya kutoa elimu. 

Msimamizi wa zoezi hilo Kaimu Afia elimu Msingi Mwl. Mathew Komba alisema zoezi hili litaendelea kwa siku tano mfululizo ambapo kwa siku ya kwanza zoezi lilifanyika katika kata tatu za Vijibweni,Kigamboni na Tungi ambapo shule 18 zilifungwa na wamiliki wa shule hizo kutakiwa kusimamisha zoezi la ufundishaji kuanzia leo tarehe 22 Agosti na endapo watakaidi hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Baadhi ya shule zilizofungwa ni pamoja na shule ya awali ya Malaika, Kigamboni English Medium school, Patmos ,Montecalos pamoja na Riziki. Zingine ni Taqwa ,Fildaus ,Mek na Charity.
Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni Ndg Stephen Katemba anatoa wito kwa wamiliki wote waliofungiwa shule kutojaribu kufungua shule hizo mpaka hapo ofisi yake itakaporidhika kulingana na maagizo yaliyotolewa.



kaimu Afisa Elimu Msingi Mwalimu Mathew Komba (Katikati) akimpa maelekezo mmiliki wa shule ya Malaika iliyopo kata ya Tungi

Wanafunzi wakiwa wamelala katika mazingira yasiyokubalika na muongozo wa usajili wa shule

Baadhi ya wanafunzi wa Kigamboni Islamik Nursery and Primary school  wakifundishwa katika jengo la Msikiti badala ya darasani