Jumatatu, 31 Julai 2017

VITUO VYA AFYA VYAPATA ALAMA ZA JUU

Mkurugenzi Bw. Stephen Katemba (kulia) akipokea taarifa kutoka kwa Bi. Ruth Ngowi          





Katika ukaguzi wa Kimaabara uliofanywa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa mwaka 2017 ,Vituo vya Afya katika Manispaa ya Kigamboni vimeonekana kuwa na alama za juu katika kutoa huduma kwa Jamii.
Katika kaguzi huo ulioongozwa na Bi.Ruth Ngowi,Jumla ya vituo vya Afya 13 vimepata alama za nyota Tatu  na zaidi ikiwa ni kiashiria kuwa huduma zinazotolewa ni bora na za kuridhisha.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni alikabidhiwa ripoti hiyo na timu ya ukaguzi na kuahidi kuendelea kusimamia ubora zaidi kwani kwa upande wa vituo vya Afya vilivyo chini yake vilikuwa na alama 76 tofauti na alama za jumla za 48 inayounganisha vituo vya serikali na vya Binafsi.
Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni ina Jumla ya Vituo vya Afya 27,kati ya hivyo 17 ni vya serikali na 10 ni vya watu binafsi na mashirika mbali mbali.

Picha ya pamoja ya watumishi wa Halmashauri na Wizara

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni